Thu, 27 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Raja Club Athletic wameongezewa bonus ya Dola 10,918 (Shilingi 25, 668, 218) endapo watafanikiwa kuwafunga na Al Ahly na kutinga hatua ya nusu fainali.
Kabla ya dau hilo, awali Raja waliwekea bonus ya Dola 7895 endapo wakiwaondosha Al Ahly katika mchezo wa pili wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika unaotarajiwa kucheza Jumamosi Aprili 29, 2023.
Kwenye mchezo wa awali ambao Al Ahly walikuwa nyumbani kwao Misri, walishinda goli 2-0 hivyo Raja anacho kibarua cha kuupanda mlima huo na kuibuka na ushindi wa zaidi ya goli 3-0.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live