Sat, 11 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Shirikisho la soka nchini Norway Lise Klaveness, amefunguka na kueleza kuwa Shirikisho la soka Duniani (FIFA) halitendi haki katika kuchagua wenyeji Kombe la Dunia.
Akizungumza na #SkyNews Klaveness ameleza kuwa maamuzi ya wapi Kombe la Dunia litachezwa kwa mwaka 2030-2034 yamefanyika kwenye mikutano ya siri iliyoongozwa na Rais wa FIFA GianniInfantino kuwa hatua zote hazikuwa za haki na uwazi.
LiseKlaveness ni mwanasheria wa Norway na mwanasoka wa zamani ambaye aliichezea timu ya taifa ya Norway ‘mechi’ 73 kutoka mwaka 2002 hadi 2011.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live