Tue, 22 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la soka Visiwani Zanzibar limekanusha Madai yaliyotolewa na Timu ya Wanawake ya New Generation ya kushindwa kuwasaidia baada ya kukwama njiani kutokana na kuishiwa fedha wakati wakitoka Nchini Uganda kushiriki Mashindano ya Afrika Mashariki na Kati kwa Timu za Wanawake CECAFA.
Timu ya Wanawake ya New Generation ilisambaza kwenye Mitandao ya Kijamii taarifa iliyotolewa na Nahodha wake, Warda Abdulhakim Mwinyi wakidai kukwama Mkoani Geita kutokana na kudaiwa na Dereva wa Gari ambalo walikuwa wanalitumia kusafiri nalo kutoka Uganda hadi Tanzania.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live