Wed, 18 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametoa bilioni 4 kwaajili ya ujenzi wa soko la kisasa la Nzega Parking mkoani Tabora ili kuwezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao kwenye mazingira bora.
Rais Dkt, Samia ametoa fedha hizo alipotembelea soko hilo kufuatia ombi la mbunge wa jimbo la Nzega na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kumuomba kutembelea soko hilo.
Aidha Rais Samia amewataka wafanyabiashara hao kupisha ujenzi na kuwaelekeza mkuu wa wilaya na mkurugenzi kuhakikisha soko likikamilika wafanyabiashara waliopisha ujenzi ndio wapewe kipaumbele.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live