Wed, 25 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan amemtambia Rais mwenzake wa Zambia, Hakainde Hichilema na kusema kuna sehemu watakuwa tofauti.
Zambia na Tanzania zimepangwa kundi F pamoja na timu za Morocco na Congo katika Mashindano ya AFCON yanayotarajiwa kuchezwa Januari 2024 nchini Ivory Coast.
“Kuna sehemu tutakuwa tofauti katika mashirikiano yetu, napo ni kwenye Timu zetu za Taifa na ziko kundi moja AFCON,“ alisema Rais Samia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live