Fri, 17 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameipongeza Timu ya Zanzibar U15 (Karume Boys) baada ya kutwaa Ubingwa wa CECAFA U15 wakiichapa Uganda katika mchezo wa Fainali kwa mikwaju ya penati 4-3.
Kupitia kurasa zake za mitandao ya Kijamii, Rais Samia ameandika;
"Hongereni sana Timu ya Taifa ya Soka ya Zanzibar kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 (Karume Boys), kwa kutwaa ubingwa wa CECAFA U15 2023. Mmetupa heshima kubwa. Nawatakia kila la kheri katika ndoto na safari yenu kwenye mchezo wa soka siku za usoni".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live