Wakati Kikosi cha Primeiro De Agosto kikitarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam leo Ijumaa (Oktoba 14) kwa ajili ya mchezo wa Mkondo wa Pili wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika dhidi ya Simba SC, Uongozi wa klabu hiyo ya Angola umewaahidi ‘DONGE NONO’ Wachezaji wao endapo watapindua meza na kutinga Hatua ya Makundi.
Wakati Kikosi cha Primeiro De Agosto kikitarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam leo Ijumaa (Oktoba 14) kwa ajili ya mchezo wa Mkondo wa Pili wa Ligi ya Mabingwa Barani Afrika dhidi ya Simba SC, Uongozi wa klabu hiyo ya Angola umewaahidi ‘DONGE NONO’ Wachezaji wao endapo watapindua meza na kutinga Hatua ya Makundi. Primeiro De Agosto itacheza mchezo wa Mkondo wa Pili Jumapili (Oktoba 16) katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, huku ikiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza nyumbani kwa mabao 3-1 mwishoni mwa juma lililopita (Jumapili-Oktoba 09).