Fri, 9 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bodi ya Ligi hii leo Agosti 9, 2024 imetangaza ratiba ya Ligi Kuu ambapo Simba wataanzia nyumbani dhidi ya Tabora United, Yanga SC wao wataanza ugenini dhidi ya Kagera Sugar.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, mechi hizo za raundi ya kwanza zitaanza kutimua vumbi Agosti 16, 2024 lakini Simba atacheza na Tabora katika uwanja wa KMC Complex Agosti 18, 2024 huku Yanga wao wakicheza na Kagera Agosti 29, 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live