Sun, 1 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Primia Ligi) 2021/2022 inaendelea leo kwa mchezo mmoja utakaopigwa katika Dimba la Sokoine Jijini Mbeya, saa 10:00 Jioni.
Wenyeji Tanzania Prisons watawakaribisha Maafande wa Polisi Tanzania ambao wanapambana kwa kila hali kuhakikisha wanaepuka janaga la kushuka daraja wana kila sababu ya kuhitaji alama tatu katika mchezo huo wa leo.
Polisi Tanzania wanahitaji alama tatu ili kuweza kufufua matumaini yao ya kukamata nafasi nne za juu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live