Wakati Michezo ya kuhitimisha michezo ya hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa Afrika, ikikamilika Jana Jumamosi April 1.
Hizi ndizo Timu nane ambazo zimekata tiketi ya kwenda hatua ya Robo Fainali ya Michuano hiyo mikubwa ya Vilabu barani Afrika
Timu zilizomaliza vinara katika makundi yao ni
Raja CA (Morocco) Mamelodi Sundowns (Afrika ya Kusini) Espérance de Tunis (Tunisia) Wydad AC (Morocco)
Timu zilizomaliza katika nafasi ya pili
Al Ahly (Misri) JS Kabylie (Algeria) CR Belouizdad (Algeria) Simba SC (Tanzania)
Droo ya kupanda michezo ya Robo Fainali itafanyika siku ya Jumatano ya April 5 Jijini Cairo nchini Misri.