Mon, 16 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Tanzania Prisons imesajili wachezaji watano wapya katika dirisha hili dogo ili kukiongezea nguvu kikosi chake kuelekea nusu iliyobaki ya msimu.
Hao ni kipa Benedict Tinocco aliyesaini miaka miwili, viungo Mohamed Ibrahimu ‘Mo’ mwaka mmoja na nusu, Shaaban Kisiga mwaka mmoja, Lambert Charlse Sabiyanka na winga Meshack Suleiman kutoka Nyasa Big Bullets ya Malawi aliyesaini miaka mitatu.
Aidha, Tanzania Prisons imewatakia kila la heri wachezaji walioondoka, kipa Hussein Abel na kiungo Mudathir Abdallah.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live