Wed, 28 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kuelekea mchezo wa Tanzania Prisons ugenini dhidi ya Simba SC, uongozi wa klabu hiyo umeweka kitita cha Tsh milioni 30 endapo Wajelajela hao wataifunga Simba SC.
Simba SC itachuana na Tanzania Prisons katika dimba la Benjamin Mkapa siku ya Ijumaa Disemba 30, 2022.
Simba inakamata nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na tofauti ya alama 6 nyuma ya vinara Timu ya Yanga.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live