Nyota wa klabu ya Azam FC, Prince Dube amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu mwishoni mwa juma huko nyumbani kwao Zimbabwe.
Mchezaji huyo ametumia muda huu wa mapumziko kuvuta jiko kabla ya kurudi kambini kujiunga na wachezaji wenzake kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu Tanzania Bara na Ule wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Dube ambae alimaliza msimu na majeruhi, ndie aliekuwa kinara wa mabao katika kikosi cha Azam FC, huku akishika nafasi ya tatu katika list ya Wafungaji bora msimu uliopita (14) akizidiwa na John Bocco (16) na Chriss Mugalu (15), wote kutoka Simba SC.