By Thomas Ng'ituMore by this Author KOCHA mpya wa timu ya Taifa ya Tanzania, Kim Poulsen leo Jumanne ametokea katika uwanja wa Uhuru kuangalia mchezo wa Ligi Kuu kati ya KMC na Mwadui.Kocha huyo alifika uwanjani hapo akiwa na gari aina ya Alphard kisha alipaki na kuanza kutafuta njia ya kuingilia uwanjani.Wakati akitafuta njia, alikutana na kocha mkuu wa Kagera Sugar, Mecky Maxime ambao nao walifika uwanjani hapo kuangalia mchezo huo kisha baadae wafanye mazoezi.Maxime alipokutana na Kim walisimama kwa takribani dakika 3 na kuzungumza mawili matatu huku wakionyeshana tabasamu.Baada ya kusalimiana na kupiga stori mbili tatu, makocha hao waliongozana na kwenda kukaa eneo la watu maalum.Kim aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Stars jana akirithi mikoba ya Etiene Ndayiragije ambaye alivunjiwa mkataba.
By Thomas Ng'ituMore by this Author KOCHA mpya wa timu ya Taifa ya Tanzania, Kim Poulsen leo Jumanne ametokea katika uwanja wa Uhuru kuangalia mchezo wa Ligi Kuu kati ya KMC na Mwadui.Kocha huyo alifika uwanjani hapo akiwa na gari aina ya Alphard kisha alipaki na kuanza kutafuta njia ya kuingilia uwanjani.Wakati akitafuta njia, alikutana na kocha mkuu wa Kagera Sugar, Mecky Maxime ambao nao walifika uwanjani hapo kuangalia mchezo huo kisha baadae wafanye mazoezi.Maxime alipokutana na Kim walisimama kwa takribani dakika 3 na kuzungumza mawili matatu huku wakionyeshana tabasamu.Baada ya kusalimiana na kupiga stori mbili tatu, makocha hao waliongozana na kwenda kukaa eneo la watu maalum.Kim aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Stars jana akirithi mikoba ya Etiene Ndayiragije ambaye alivunjiwa mkataba.