Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Pogba atafunwa na skendo ya 'kumroga' Mbappe, kaka'ke aanika mazito

Pogba Family Ml Pogba

Thu, 1 Sep 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mathias Pogba, kaka mkubwa wa Paul Pogba ameshiriki video mpya akishikilia madai yake kuwa nyota huyo wa zamani wa Man United alihusika katika uchawi. Kiungo huyo wa Juventus, amekutwa na kisa cha jaribio la unyang'anyi wa fedha kiasi cha pauni 13 milioni.

Pogba amekanusha vikali tuhuma za kaka yake kwamba anajihusisha na uchawi naye Mbappe anaendelea kufuatilia kwa karibu sakata hiyo.

Mathias Pogba amefichua madai mengine ya kushtua dhidi ya mdogo wake ambaye ni kiungo wa kati wa Juventus, Paul Labile Pogba huku mgogoro kati ya ndugu hao ukiendelea.

Mathias aliwasha moto mtandao wa kijamii na video yake ya dakika tatu siku ya Jumapili, Agosti 28, akiahidi kuchapisha "ufichuzi mkubwa" kuhusu nyota huyo wa zamani wa Manchester United.

Paul kwa majibu yake ya haraka kupitia kwa mawakili wake alidai kuwa kaka yake ni mmoja wa genge la uhalifu lililopangwa kumlaghai kitita cha Pauni milioni 13.

Lakini katika kuongezea chumvi kwenye jeraha, kaka mkubwa wa Pogba alifichua kuwa mshindi huyo wa Kombe la Dunia mwaka wa 2018, amekuwa akitumia mamilioni ya pesa katika uchawi ili kujilinda dhidi ya kupata jeraha.

Mathias alishiriki video mpya, akifafanua zaidi ufichuzi wake wa "mlipuko" kuhusu Paul, ambaye kwa sasa anauguza jeraha.

"Kutokana na hayo, njia pekee ya kujinusuru ambayo mimi [Mathias] ninayo ni kufichua uwongo wake [Paul] na udanganyifu wake," alisema kama alivyonukuliwa na Get French Football News.

“Ndiyo maana nilithibitisha uchawi wake kwa sababu cha muhimu hapa si kwamba iwapo inafanya kazi au uniamini au usiniamini, ni kwamba ina nia mbaya kwa sababu uchawi huu unategemea kufanya mambo mabaya kwa matambiko yao kwa nia ya kudhuru."

"Pia, ninauliza, je, hivi Paul hakukataa kukimbilia kwa waganga? Sasa kwa nini alifichua hilo kwa mpelelezi? Pogba alikiri kwa polisi kuwa alimlipa mganga katika msafara wake kujikinga na majeraha."

"Je, kujikinga na majeraha kunahitaji kulipa mamilioni ya euro kwa mchawi huyu kwa miaka? (hasa kwa vile haikufanya kazi)," alimaka.

Hata hivyo, Paul Pogba amekanusha vikali tuhuma za kaka yake kwamba anajihusisha na uchawi. Jina la Kylian Mbappe pia limekuwa likitajwa mara kwa mara katika sakata inayoendelea kati ya Paul Pogba na kaka yake. Mathias alifichua kwamba Pogba amekuwa akitumia uchawi kwa Mbappe.

Katika taarifa iliyonukuliwa na gazeti la Sun, Mathias alisema: "Kylian, sasa unaelewa? Sina chochote kibaya dhidi yako, maneno yangu ni kwa manufaa yako, kila kitu ni kweli na kuthibitishwa, na inajulikana! Pole kwa haya kaka, anayejiita Muislamu yuko ndani ya uchawi. Sio vizuri kuwa na mnafiki na msaliti karibu na wewe!"

Inaripotiwa kwamba Mbappe na wawakilishi wake wanafuatilia kwa karibu sakata hiyo. Inaaminika kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 23, anaweza kuchukua hatua iwapo atasukumwa. Lakini hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kutoka kwake huku polisi wakiendelea na uchunguzi.

Kwa upande wake, Pogba amejitete akisema; "Ni kweli nilimlipa pesa mganga wa jadi, lakini nilifanya hivyo ili anisaidie kuepukana na majeraha ya mara kwa mara, sikumlipa Mganga ili amroge Kylian Mbappe," amesema Pogba akiwa Polisi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live