Kocha wa klabu ya Paris Saint Germain Mauricio Pochettino amekataa kutoa lawama kwa mwamuzi alichezesha mchezo wao dhidi ya Nantes siku ya jumamosi na kupoteza kwa goli 3-1 kwenye dimba la Stade de la Beaujoire.
Nantes walikuwa kwenye ubora wa hali ya juu hasa kwenye kipindi cha kwanza na kufanikiwa kupata goli tatu zote ambazo zilifungwa na Randal Kolo Muani, Quentin Merlin na Ludovic Blas
Wakati akihojiwa na waandishi Pochettino alinukuliwa akisema, “tulifanya shambulio letu la kwanza kupitia Juan Bernat lakini walitufunga kwenye shambulio lililofuata, tulijaribu mara mbili kwenye muda wa majeruhi, tulifanya mashambulizi mazuri, lakini hatukuwa na udhibiti mzuri wa nafasi ya ulinzi hii ni pamoja na makosa mengi tuliyoyafanya.
“Inabidi tutenganishe hili, Hatukupoteza kwa sababu ya referee, naweza kuelewa shinikizo la wachezaji wangu na mkurugenzi, ungeweza kurudia mchezo, lakini haimaanishi kuwa ndio sababu ya kupoteza.”