Tue, 25 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya FC Platinum imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Zimbabwe 'Castle Lager Premiership' kwa msimu wa nne mfululizo.
FC Platinum wametwaa ubingwa huo baada ya kumaliza Ligi msimu wa 2021/22 wakiwa na alama 68 katika michezo 31 waliocheza, wakipata ushindi mechi 20, sare mechi 8 na wakipoteza mechi 3.
Hii ni mara ya tatu kwa kocha Norman Mapeza kushinda Ligu kuu ya Zimbabwe akiwa na klabu ya Platinum na mara yake ya nne akiwa nchini Zimbabwe.
Mapeza alishinda Ligi Kuu ya Zimbabwe kwa mara ya kwanza akiwa na klabu ya Monomotapa mnamo 2008.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live