Pitso Mosimane timu Kwa sasa tangu aondoke Al Wahda, Kaizer Chiefs wanataka kocha huyu atue ndani ya timu yao Ili akawatengenezee timu ya kutikisa hapa Afrika.
Hata hivyo Pitso Mosimane aliwahi kusema hatafanya kazi sehemu tofauti na Mamelodi Sundowns pale Kwa Madiba, kwa hiyo tusubiri kuona ushawishi wa mabosi wa Kaizer Chiefs Kwa Kocha huyu mwenye mafanikio makubwa hapa Afrika.
Mosimane hawezi kutua ndani ya timu yako kama hauna project ya kueleweka kocha huyu anataka kufundisha timu ambayo itamfanya aendelee kuwa tishio katika medani ya Soka.
Pitso Mosimane ni zao la Mamelodi Sundowns kama Rhulani Mokwena Kwa sababu Ulimwengu wa Soka umewatambua ndani ya Klabu hii yenye maskani yake Pretoria.