Tue, 8 Feb 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mambo yameiva pale Zambia. Mshambuliaji hatari Moses Phiri ???????? amefunguka kwamba msimu ujao anatua Msimbazi baada ya makubaliano ya awali kufanyika
“Bado mimi ni mchezaji wa Zanaco, lakini kama Simba wamekuja na ofa nzuri mezani kwa nini nikatae wakati mpira ndio kazi yangu.”
“Uwepo wa Chama na Bwalya katika kikosi cha Simba kimenifanya niridhike kuwa, kikosi cha timu hiyo kinaundwa na mastaa wanaotaka mafanikio.”
“Naongea sana na Chama ni rafiki yangu sana ameniambia nipambane kuhakikisha nakuja huko, nafatilia mechi nyingi za Simba ni timu kubwa.” Amesema Phiri. Via [Goal Africa]
Chanzo: www.tanzaniaweb.live