Mon, 16 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Rangers imemteua Kocha Mkuu wa zamani wa Monaco Philippe Clement kuwa Meneja wao mpya kwa mkataba wa miaka mitatu na nusu.
Clement (49) ambaye ni mlinzi wa zamani wa Ubelgiji, alifukuzwa kazi na Monaco mwezi Juni baada ya kuongoza kwa miezi 18.
Anachukua nafasi ya Michael Beale aliyefukuzwa kazi mapema mwezi huu.
Mwenyekiti wa Rangers John Bennett amesema kuwa walijipanga na kufuata hatua za kina za uajiri na mbelgiji huyo ni bora na anayewafaa kwa kila kiwango.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live