Baada ya kuzuka tetesi kuhusiana na ‘klabu’ ya Chelsea kutaka kumsajili ‘kocha’ Jos eMourinho, mchezaji wa zamani wa Chelsea na Arsenal Emmanuel Petit ametoa ushauri kwa ‘timu’ hiyo kwa kudai kuwa uwamuzi huo siyo sahihi
Kwa mujibu wa The Sun News inaelezwa kuwa Petit ambaye aliwahi kuichezea ‘klabu’ hiyo kutoka mwaka 2001 hadi 2004 anaamini kuwa Chelsea inahitaji ‘kocha’ atakaeirudisha ‘timu’ hiyo katika ubora wake.
Mbali ya kumkataa Mourinho, Petit ametaja baadhi ya ma-kocha ambao anaona wanweza kuwa chaguo sahihi kwa ‘klabu’ hiyo akiwemo ‘kocha’ wa Arsenal Mikel Arteta.
Wazo la kusaka ‘kocha’ mpya ‘klabuni’ hapo linakuja baada ya mashabiki kumkataa ‘kocha’ mkuu Mauricio Pochettino kutokana na matokeao mabovu anayoyapata.