Klabu ya Como FC inayonolewa na kiungo wa zamani wa Arsenal, Barcelona na Chelsea, Cesc Fàbregas imekamilisha usajili wa mlinda mlango wa zamani wa Liverpool, Pepe Reina kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Klabu ya Como FC inayonolewa na kiungo wa zamani wa Arsenal, Barcelona na Chelsea, Cesc Fàbregas imekamilisha usajili wa mlinda mlango wa zamani wa Liverpool, Pepe Reina kwa mkataba wa mwaka mmoja. Reina (41) raia wa Uhispania ambaye alianza maisha yake ya soka kwenye shule ya vipaji ya Barcelona almaarufu La Masia amewahi kuvitumikia vilabu vya Barcelona, Villarreal, Liverpool, Napoli AC Milan, Aston Villa, Lazio na Villarreal.