Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Pep Guardiola atupa kijembe Kombe la Dunia

Pep Guardiola Qatar Pep Guardiola

Thu, 10 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Pep Guardiola amekashifu Uamuzi wa Kombe la Dunia kuandaliwa Qatar na kusema hatawalaumu wachezaji wake kwa kuvurugwa, kwani rais wa zamani wa FIFA Sepp Blatter alikiri kwamba kuichagua Qatar kama wenyeji ni ‘kosa’.

Manchester City inayonolewa na Guardiola iliikaribisha Chelsea katika raundi ya tatu ya Kombe la Carabao jana Jumatano na Brentford katika Ligi ya Uingereza Jumamosi, na meneja huyo alisema atatazama kuona kama wachezaji wake wanaogopa majeraha.

“Tuna Kombe la Dunia na wachezaji hawawezi kupumzika,” alisema. “Wachezaji wana jicho moja kwenye Kombe la Dunia. Ikiwa utapata jeraha dhidi ya Brentford, haitabadilisha chochote kuhusu kushinda EPL au la, lakini utakosa Kombe la Dunia.

“Ilinibidi kuwaambia vijana kuwa makini mwezi mmoja uliopita, lakini sasa ni karibu. Tunacheza Jumamosi na Jumapili lazima wawe na timu ya taifa.

“Nina hakika hilo litakuwa akilini mwa wachezaji. Ningekuwa vilevile.” Alisema Guardiola.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live