Tue, 23 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Man City Josep Pep Guardiola amesifu kiwango cha mlinzi wake Nathan Ake na nafasi ya ulinzi msimu huu:
Pep Guardiola:
“Nimejifunza msimu huu unapocheza dhidi ya Bukayo Saka, Vinicius Junior, Gabriel Martinelli au Mohamed Salah, unahitaji mabeki wazuri kushinda mechi moja moja.
“Nathan Ake amekuwa wa msingi kwetu. wanahitaji hatua moja tu kukupiga. Nathan alitupa nguvu ambayo hatukuwa nayo hapo awali.”
Ake amekuwa na msimu bora na tayari ameshanyakua taji la EPL akiwa na Manchester City.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live