Mon, 19 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amekana klabu yake kumuhitaji nyota wa PSG Kylian Mbappe.
Mbappe ambae anatajwa kuwekwa sokoni na PSGikiwa kuna Klabu itakayopanda dau Mkataba wake na PSG umebakiza mwaka mmoja na ameweka wazi kuwa hataongeza Mkataba mpya.
Mara kwa mara Mbappe ameweka wazi nia yake ya kujiunga na miamba wa Ulaya Real Madrid.
Akizungumzia uhamisho wa Mbappe kutua Man City Pep amesema;
"Hatutamsajili Mbappe wala hatujaonesha nia ya kumuhitaji na kubwa zaidi wote mnafahamu ni wapi anapahitaji ikiwa ataondoka PSG"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live