Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Pep Guardiola akutana na Declan Rice

Man City829.png Pep Guardiola akutana na Declan Rice

Thu, 29 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha wa Mabingwa wa Soka nchini England Manchester City, Pep Guardiola, ameamua kukutana uso kwa uso na kiungo wa West Ham United, Declan Rice ikiwa ni sehemu ya kumshawishi kutua klabuni hapo na kuachana na mpango wa kwenda Arsenal.

Hii ni baada ya West Ham United kukataa ofa ya kwanza ya Manchester City ambayo walipeleka kiasi cha Pauni 80m sambamba na fedha ya ziada Pauni 10m.

Wakati Man City wakipeleka ofa hiyo, Arsenal wameshapeleka ofa mara tatu kwa West Ham na zote zimekataliwa.

Kutokana na hilo, hivi sasa vita imebaki kwa Man City na Arsenal juu ya kumuwania nyota huyo wakati West Ham United wakisema dau la Rice ni pauni 100m.

Imeelezwa kuwa, Guardiola alikutana na Rice na kuzungumza naye uso kwa uso kumshawishi kutua ndani ya kikosi hicho na sio kwenda timu nyingine.

Inaelezwa kuwa, hata Mikel Arteta alishajaribu kumshawishi Rice na kumuhakikishia atakuwa mchezaji muhimu ndani ya kikosi chake, lakini hadi sasa bado hakijaeleweka.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live