Sun, 8 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Pep Guardiola amekataa ofa ya kuwa Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Brazil kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia 2026.
Ripoti zinadai kuwa Legend wa Brazil, Ronaldo amefanya mazungumzo na wakala wa Guardiola, Pere kwaajili kuchukua nafasi hiyo lakini amekataa.
Guardiola (51) amekuwa na mafanikio makubwa kwenye klabu alizofundisha huko Hispania, Ujerumani na sasa England.
Kandarasi mpya ya Guardiola na Man City ni ya miaka miwili ambapo itafikia tamati 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live