Tue, 12 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Man City Pep Guardiola amesema kuwa anashangazwa na kauli za wale wanaosema Timu yake haina uwezo wa kugombea Ubingwa wa EPL msimu huu.
Akizungumza Pep ambae ameishuhudia City ikipata matokeo hafifu katika micezo mitatu mfululizo kabla ya kuibuka na ushindi wikiendi iliyopita anasema;
"Watu wanasema Man City tayari tumeisha lakini tunataka kuwakosoa na kuwaaminisha kwamba ngoma bado haijaisha, bado tunataka kuendelea kutoa changamoto. Kuhusu kufanikiwa katika hilo itategemea na namna tutakavyocheza." Amesema Pep Guardiola,
Chanzo: www.tanzaniaweb.live