Mkongwe wa Wafalme wa Soka duniani, Brazil, Pele ameondolewa Hospitalini baada ya kupewa vipimo vya matibabu.
Mshindi huyo wa Kombe la Dunia mara tatu mwenye umri wa miaka 81, alifanyiwa upasuaji wa uvimbe mwezi Septemba ingawa tena Waganga katika Hospitali hiyo walisema walihitaji pia matibabu ya chemotherapy.
“Pele ameimarika, na ataendelea na matibabu”, ilisema taarifa ya Hospitalini hapo.
Pele ambaye anashikilia nafasi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote Brazil akiwa na goli 77 katika mechi 92, alilazwa katika Hospitali hiyo tangia Agosti 31 baada ya uvimbe kungunduliwa kwenye njia ya utumbo.