Mchezaji wa zamani wa Simba SC na timu ya Taifa Tanzania, Boniface Pawasa amesema moja ya fursa zilizopo kwa Tanzania kuandaa Afcon 2027 ni kuingiza kipato kama nchi.
Pawasa amesema vyema kuanza kujiandaa kwenye viwanja na sio vya mechi pekee kwasababu vitahitajika vya mazoezi na kambi hivyo tutanufaika navyo.
"Isiishie kwenye kushiriki pekee, tuweke maandalizi maana kwenye mpira miaka minne michache kutoka 2023, uenyeji wetu tunatakiwa mmoja katika nchi zetu icheze fainali, itakuwa huzuni kushuhudia fainali inachezwa mataifa mengine,"
Amesema Pawasa akichangia mjadala wa X Space ulioandaliwa na Mwananchi Communications Limited (MCL)