Mchezaji wa zamani wa Simba Boniface Pawasa amesema kuwa ana uhakika wa asilimia zote kuwa Simba atashinda kwenye mechi yao dhidi ya Yanga huku akisema yeye tayari ameshawabetia Simba na ameweka shilingi laki moja.
Mchezaji wa zamani wa Simba Boniface Pawasa amesema kuwa ana uhakika wa asilimia zote kuwa Simba atashinda kwenye mechi yao dhidi ya Yanga huku akisema yeye tayari ameshawabetia Simba na ameweka shilingi laki moja. Pawasa amesema haya; "Naiheshimu Yanga, wanacheza vizuri lakini kwenye mechi ijao ya Derby karata yangu naiweka Simba sina wasi wasi na hilo na tayari nimeshabeti nimeweka laki moja mahali. Juzi nilikua na watu wa Yanga wanakiri Simba iko mbali inafanya mambo makubwa," amesema Pawasa.