Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua Kim Paulsen, raia wa Denmark kuwa kocha wa Timu ya Taifa ‘Taifa Stars’.
Taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Mario Ndimbo, imesema kocha huyo amesaini mkataba wa miaka mitatu kuifundisha Taifa Stars, ambayo kwa sasa inawania nafasi ya kucheza Fainali za AFCON, Kombe la Dunia la 2022.
Paulsen aliwahi kuinoa Taifa Stars kati ya 2012 na 2013 ambapo kabla ya kupewa nafasi hiyo alikuwa kocha wa timu za Taifa za vijana.
Kocha huyo anachukua nafasi ya Etienne Ndayiragije aliyefungashiwa virago baada ya kuifundisha timu hiyo tangu Julai 2019.