Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Paul Pogba anakipiga popote tu hata Uingereza

Paul Pogba Kiungo wa Manchester United, Paul Pogba

Thu, 17 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo wa klabu ya Manchester United ambaye mkataba wake unaisha majira ya kiangazi Paul Pogba amefungua milango kwa vilabu vya Uingereza ambavyo vitahitaji huduma yake kuwa yuko tayari kusikiliza offer zao.

Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka nchini Ufaransa, amebakisha miezi minne tu kwenye mkataba wake ambao June 30 ndio unamalizaka na kuwa mchezaji huru, awali alisema kuwa kwa sasa anataka kujikita kwenye kuboresha afya yake baada kupata majeruhi na hakuwa tayari kuamua lolote.

Paul Pogba majira ya kiangazi atakuwa ni moja ya majina makubwa ambao watakuwa huru, ikiwa ataamua kuachana na Man Utd baada ya kuitumika kwa miaka sita tokea alipojiunga akitokea Juventus kwa uhamisho wa £89.3million atakuwa moja pigo kubwa sana kwa klab hiyo.

Paul Pogba kwa sasa anangalia uwezekano wowote ambao utamnufaisha yeye, kwani ni klabu chache sana ambazo zinaweza kumudu kumlipa mshara wa £290,000 kwa wiki, na kisa cha kufungua milango kwa vilabu vya Uingereza ni sababu kuna idadi kubwa ya vilabu vinavyoweza kumudu kumlipa mshahara huo.

Awali vilabu vya Chelsea na Manchester City kila moja ilitaka kupata huduma yake kwa vipindi tofauti wakati akiwa anakipiga nchini italia kwenye klabu ya juventus.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live