Nyota wa zamani wa AC Milan Alexandre Pato anasema familia yake ndio kitu kinachompa furaha zaidi na mpira haujawahi kumpa furaha kama watu wengi wanavyofikiri na kuhusu Ballon D’Or , yeye anamuhesabu mke wake kama tuzo .
“Kadri unavyokua mkubwa ndio unatambua ni nini kinafanya uwe na furaha !”
“Wakati naondoka nyumbani, nilifikiri soka lilikuwa na kila kitu nilichotaka , nilikwenda Italia, Uingereza, Hispania, China huko kote niliteseka, nililia, nilipata maumivu na kote nilikuwa mpweke “
“Pengine sikuwa mchezaji bora zaidi duniani lakini wacha nikuambie kitu,nina amani sana na familia yangu na nafsi yangu “
“Nina mke ninayempenda sana anafanya nijione ni mwenye Ballon d'Or nyingi na kama maisha ni mchezo, basi nimeshinda kila kitu.”