Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Pamba yapiga honi Ligi Kuu, yaichapa Nyamagana bao 4

Pamba Jiji FC CHAM Pamba yapiga honi Ligi Kuu, yaichapa Nyamagana bao 4

Mon, 22 Jan 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wenyeji, Pamba FC jana waliibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Mwana Stand United katika mchezo wa Ligi ya NBC Champonship Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Mabao ya Pamba FC yalifungwa na Mudathir Said, Hassan Mwasapili, Haruna Chanongo na Lazaro Mlingwa, wakati bao pekee la Stand United lilifungwa na Lucas Sesana.

Mechi nyingine za jana za Ligi ya NBC Championship, Mbuni FC iliichapa Pan Africans mabao 3-1 Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijjini Arusha na Mbeya City ikawatandika Mbeya Kwanza 4-2 Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.

Ligi ya NBC Championship itaendelea leo kwa michezo mingine mitatu; TMA na Cosmopolitan Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha, COPCO na Biashara United Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na Ken Gold na Ruvu Shooting Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Msimamo wa NBC Championship ni Pamba FC kileleni pointi 40 mechi 18, ikifuatiwa na Ken Gold pointi 39 mechi 17.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live