Game changer ni Pacome, wakati huyu jamaa anakwenda kupiga penati ya tatu, wachezaji, benchi la ufundi na mashabiki walikuwa wamekata tamaa na wakati huo Yanga walikuwa nyuma kwa penati mbili, Pacome alikaza moyo akachagua angle na kupiga penati ya ufundi dhidi ya kipa mgumu wa Azam.
Baada ya kufunga alimfuata Kipa wake Diarra akampatia mpira na kumpa maneno ya hamasa,binafsi sikujua kamwambia nini ila kwa vitendo Pacome alimchochea sana Diarra kisha akawambia mashabiki wa Yanga jukwaani ambao wamekata tamaa washangilie.
Ile ndo ilikuwa turning point kwa Yanga, Pacome alifufua confidence ya timu nzima,mpira ni mchezo wa akili na Pacome kalifanya hilo jambo kwa usahihi.