Thu, 15 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Pacome Zouzoua amesema amejipanga kivingine kwani ana kiu ya kufanya makubwa zaidi akiwa na Yanga hususani katika mechi za kimataifa atakazoshiriki kwa msimu wa tatu mfululizo moja akiwa na Asec.
“Kila mchezaji wa kikosi chetu hataki kufanya makosa anapopewa nafasi kwani wote ni bora, jambo ambalo linaongeza ushindani mkubwa zaidi
“Sioni kama kuna jambo litatushinda msimu ujao, kwani mipango yetu sio kubeba makombe tu kama tulivyoanza na Ngao ya Jamii tuliyoikosa mwaka jana, pia kuwafurahisha mashabiki na viongozi kwa ujumla.”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live