Tue, 28 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya msimu uliopita kupigwa nje ndani na kushindwa kufika fainali na Man City , PSG wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani Parc De Princes wameiadhibu City magoli 2-0.
katika mchezo huo kama ilivyo ada kwa Lionel Messi anapokutana na Vilabu vya Uingereza na hasa Arsenal na Man City ametupia bao moja 74' na kufungua akaunti yake ya magoli ndani ya kikosi hicho.
Goli jingine la PSG limefungwa na Kiungo Gueye 8',na kuwahakikishia PSG kuondoka na pointi 3.
kwa matokeo hayo,PSG amefikisha Pointi 4 akiongoza Kundi A, sawa sawa na Clubb brugge.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live