Wed, 20 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Wanajangwani, Yanga, kimewasili Jijini Dar es Salaam, Kutokea kule Mkoani Ruvuma walipokwenda kucheza mechi yao dhidi ya KMC.
Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa Maji maji Songea, umewashuhudia Yanga wakiondoka na alama tatu baada ya kuishindilia KMC kipigo cha magoli 2-0.
Ktika mchezo huo magoli ya Yanga yamefungwa na Fiston Mayele pamoja na kiungo Feisal Salum.
Katika taarifa yake Yanga imesema kwa sasa wanatazama maandalizi kuelekea mechi ijayo dhidi ya Azam FC, itakayopigwa Oktoba 30.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live