Fri, 5 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nahodha wa zamani wa Barcelona Xavi Hernandez anasafiri kuelekea nchini Hispania kwenda kuchukua jukumu la kukinoa kikosi cha Barcelona.
Barca ambayo imeamua kuachana na kocha wao Ronald Koeman wiki iliyopita alikua kwenye mazungumzo ya kukabidhiwa kikosi hicho na amekubaliana na majukumu hayo.
Xavi ambae alikua anakinoa kikosi cha Al-Sadd ya nchini Qatar, anakwenda Barcelona huku ikiwa haijawekwa wazi atapewa kandarasi ya muda gani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live