Fri, 8 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya Siku ya Jana kuwachakaza Wagosi wa Kaya, Coastal Union Kikosi cha Simba kimesafiri kuelekea mjini Moshi kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Polisi Tanzania.
Mchezo huo utapigwa April 10 katika Uwanja wa Ushirika mjini Moshi na baada ya hapo Simba watakuwa na Kibarua dhidi ya Orlando Pirates mchezo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika.
Simba walipata mapokezi makubwa walipofika mjini Moshi huku Mashabiki wakijitokeza kwa wingi barabarani.
Tazama hapa chini Kikosi hiko kikiwasili Moshi;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live