Wed, 13 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shamra shamra za wiki ya hamasa kwa upande wa wekundu wa Msimbazi, Simba SC bado zinaendelea kusimamisha mji baada ya hii leo Aprili 13 kuiteka ferry na maeneo ya Kigamboni.
Meneja wa Habari wa Simba na wanachama walianzia safari yao Ferry Jijini Dar wakapanda pantoni mpaka Kigamboni walipokwenda kupeleka hamasa kisha wakarejea tena Ferry.
Hizi ni shamra shamra kuelekea mchezo wa Robo Fainali Kombe la Shirikisho dhidi ya Orlando Pirates utakaopigwa Aprili 17 katika uwanja wa Benjamin Mkapa.
Tazama picha hapa chini kuona shamra shamra zilivyokuwa;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live