Sun, 7 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya JS Kabylie ya Algeria imeonyesha nia ya kutaka kumsajili Willy Onana anayekipiga katika klabu ya Simba SC.
Taarifa zinasema kuwa ofa itatumwa wiki ijayo kujaribu kutupa ndoano ya kumnasa mchezaji huyo.
Mbali ya mchezaji huyo klabu hiyo inamsaka Abedi Bigirimana kiungo anayekipiga katika timu ya Police FC ya Rwanda.
Abedi Bigirimana mchezaji wa timu ya taifa ya Burundi kwa mwaka uliopita ndiye aliyepachika mabao mengi akiifungia Inatmba Murugamba mabao sita.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live