Mon, 23 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Willy Onana, ametoa kauli ya kishujaa kueleka mchezo wao marudiano dhidi ya Al Ahly hapo kesho Oktoba 24, 2023.
Onana ametoa kauli hiyo ameitoa leo akiwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari kuelekea kwenye mechi hiyo ya African Football League utakaopigwa nchini Misri.
“Mpira ni mchezo wa wazi na wala si rekodi za nyuma. Kwetu tumefanya maandalizi ya kutosha kulingana na mahitaji ya mchezo wa kesho yalivyo na lengo letu kubwa ni kuhakikisha tunapata matokeo mazuri. Hali na morali ya wachezaji wenzangu zilivyo juu hili linawezekana kulitimiza,”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live