Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Onana akwea pipa, aiwahi Wolves

Andre Onana Ndege Onana akwea pipa, aiwahi Wolves

Mon, 29 Jan 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Nyanda wa Manchester United na Cameroon, Andre Onana yupo safarini kurejea England tayari kwa kuendelea na majukumu yake na Mashetani Wekundu baada ya Cameroon kusukumizwa nje ya AFCON 2023.

Meneja wa Man United, Eric Ten Hag amethibitisha kuwa kipa huyo wa zamani wa Barcelona, Ajax na Inter Milan atakuwa sehemu ya kikosi chake kitakachoikabili Wolves siku ya Alhamisi.

Onana alikuwa sehemu ya kikosi cha Cameroon kilichofuzu hatua ya 16 bora ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2023 kabla ya kuondoshwa kwenye hatua hiyo kufuatia kipigo cha 2-0 dhidi ya Nigeria.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live