Baada ya mchezo kumalizika Kocha mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema mchezaji wao Augustine Okrah alipata jeraha la kichwa dakika ya 58 ‘ hivyo alishindwa kuendelea na mchezo na kwa wakati huo hakuwa sawa lakini kwa sasa yupo vizuri kiasi
Licha ya hivyo Gamondi ameongeza kwa kusema Klabu inaendelea na taratibu zake za kawaida inapotokea ajali kama hii, hivyo Okrah atapelekwa hospitali kwa uchunguzi na matibabu zaidi.
Okrah alishindwa kung'ara akiwa na Simba misimu kadhaa iliyopita baada ya kuitumikia klabu hiyo na kuandamwa na majeraha huku pia akitajwa kuwa na tatizo la utovu wa nidhamu.