Thu, 8 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota mpya ndani ya Kikosi cha Yanga, Augustine Okrah aliyeumia kwenye michuano ya Mapinduzi Cup mapema Januari, mwaka huu, sasa amerejea na yupo tayari kuivaa Mashujaa.
Okrah anatarajiwa kuwepo leo Alhamisi katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Mashujaa utakaochezwa saa 1:00 usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Kiungo huyo akicheza itakuwa ndio mchezo wake wa kwanza wa ligi akiwa na jezi ya Yanga tangu ajiunge nasi Desemba mwaka jana akitokea Bechem United ya nchini Ghana.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live