Sun, 16 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Benchem United ya Ghana imepanga kumrejesha nyumbani winga wa Yanga, Augustine Okrah aliyeonekana kutokuwa katika mipango ya kocha Miguel Gamondi.
Imeripotiwa Waghana wamefungua milango kwa winga huyo aliyefanya vizuri akiwa na timu hiyo kabla ya kurejea Tanzania wakati wa dirisha dogo, awali aliichezea Simba.
Ikumbukwe Kocha Wa Yanga SC, Miguel Gamondi ameshaweka bayana kuwa Winga huyo hatakuwa sehemu ya Mipango yake kuelekea Msimu ujao wa 2024-25.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live