Wed, 28 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa zamani wa klabu ya Chelsea, John Obi Mikel (35) ametangaza kustaafu soka baada ya miaka 18.
Kiungo huyo kutokea Nigeria alikuwa Stamford Bridge kwa miaka 11 na baadae kwenda kwenye timu zingine, hivi sasa alikuwa akiichezea Kuwait SC.
Kupitia mtandao wa Instagram, Mikel aliandika kuwa; "Kuna msemo unasema vitu vyote vizuri ni lazima vifikie mwisho, na kwa kazi yangu ya soka la kulipwa, kwangu siku hiyo ni leo".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live