Sun, 11 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa kimataifa wa Tanzania, Amahl Pellegrino amejiunga na Klabu ya San Jose Earthquakes inayoshiriki Ligi kuu nchini Marekani.
Pellegrino amesajiliwa akitokea Klabu ya FK Bodo/Glimt ya nchini Norway ambapo msimu uliopita alifanikiwa kuwa kinara wa Ligi hiyo kwa upachikaji wa magoli.
Pelle alikuwa miongoni mwa nyota walioitwa kwenye kikosi cha awali na kocha mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kwaajili ya kuiwakilisha nchi kwenye fainali za AFCON.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live